Jamaa mmoja toka bushi aliingia mjini na kufikia kwa ndugu yake, katika tembea tembea yake alimtembeza sehemu zote muhimu kama Kariakoo mtaa wa Kongo na Soko la Karume.
Baada ya kulifahamu jiji kidogo, siku moja alimuomba ndugu yake pesa aende akanunue vitu. Ndugu yake baada ya kumpa pesa, alimueleza;
“Unajua mjini wanauza nguo kulingana na muonekano wako, sasa mtu akikuuzia nguo usikubali moja kwa moja, komaa naye akupunguzie lazima utanunua kwa bei ndogo.”
Baada ya maelekezo jamaa aliingia mitaa ya Mchikichini na kukutana na jamaa anauza viatu.
“Viatu bei gani?”
“Elfu 22.”
“Aah, nipunguzie bwana.”
“Leta basi ishirini.”
“Nipunguzie bwana.”
“Wewe mnunuzi kweli?”
”Ndiyo.”
“Basi leta 15.”
“Nipunguzie bwana.”
“Bei ya mwisho 10.”
“Nipunguzie bwana.”
“Kila bei nikupunguzie, basi chukua bure.”
“Aah, nipunguzie bwana.”
Muuza mitumba aliamini yule jamaa hakuwa mzima anapoomba apunguziwe hata bure. Hii kali, jamaa avunja rekodi ya kupunguziwa.
“Unajua mjini wanauza nguo kulingana na muonekano wako, sasa mtu akikuuzia nguo usikubali moja kwa moja, komaa naye akupunguzie lazima utanunua kwa bei ndogo.”
Baada ya maelekezo jamaa aliingia mitaa ya Mchikichini na kukutana na jamaa anauza viatu.
“Viatu bei gani?”
“Elfu 22.”
“Aah, nipunguzie bwana.”
“Leta basi ishirini.”
“Nipunguzie bwana.”
“Wewe mnunuzi kweli?”
”Ndiyo.”
“Basi leta 15.”
“Nipunguzie bwana.”
“Bei ya mwisho 10.”
“Nipunguzie bwana.”
“Kila bei nikupunguzie, basi chukua bure.”
“Aah, nipunguzie bwana.”
Muuza mitumba aliamini yule jamaa hakuwa mzima anapoomba apunguziwe hata bure. Hii kali, jamaa avunja rekodi ya kupunguziwa.
No comments:
Post a Comment