Wednesday, December 14, 2011

HADITHI HADITHI!!

HADITHI NJOO UTAM KOLEA.
Hapo  zamani  za kale alitokea jamaa mmoja katika  kijiji  chao  alisifika  kuwa
 na  roho  mbaya sana.  Sifa  hizo  za  roho  mbaya  zikamfikia   mfalme
wa  kijiji  chao.  Hivyo  katika  sherehe   kubwa  aliyoindaa  kwa
ajili  ya  kusherekea  mavuno  mfalme  akamwalika  jamaa  na   kukaa
nae  mezani.   Mwisho  wa ile  sherehe  mfalme  akamuuliza  jamaa
mbele  ya hadhira.
Mfalme"   kijana  naomba  uombe  kitu  kimoja  tu.  lakini  kila
utakachoomba  kimoja  ndugu  yako   nitampa  viwili  zaidi  yako"
jamaaa  akafikilia  sana  na  akajibu
jammaa"  mheshimiwa  mfalme  naomba  nitobolewe  jicho  langu  la
kushoto" .  Mfalme  akaguna  na  akasema,
mfalme: "  du  kweli  wewe  una roho  mbaya  hivyo  naamrisha
maaskari  wakukamate  na  wakakutupe   gerezani. Kwa  maana kuwa
ukitobolewa  jicho  moja  nduguyo  atatobolewa  yote  mawili   na
nimeamini  kuwa  una roho  mbaya.
Mtu mwenye  roho  mbaya  mwisho  wake ni  majuto  na  kuona  kuwa
anaonewa.  Mwisho  wake upo    lakini   unaweza  kuchelewa  tu  kwa
sababu  moja  au  nyingine.  akitendwa  huwa  analalamika  sana.
Regards

No comments: